فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.


فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.


فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.


هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.


نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?


أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?


ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?


نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi


عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.


وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?



الصفحة التالية
Icon