فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!


فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama usiku wa giza.


فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Asubuhi wakaitana.


أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.


فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,


أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.


وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.


فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!


بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali tumenyimwa!


قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?



الصفحة التالية
Icon