وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.


لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.


فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ

Basi naapa kwa mnavyo viona,


وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ

Na msivyo viona,


إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.


وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.


وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.


تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.


وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ

Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,


لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,



الصفحة التالية
Icon