وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا

Na inapo mgusa kheri huizuilia.


إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ

Isipo kuwa wanao sali,


ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wanadumisha Sala zao,


وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu


لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;


وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,


وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.


إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.


وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao.


إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -



الصفحة التالية
Icon