ثُمَّ إِنِّي دَعَوۡتُهُمۡ جِهَارٗا

Tena niliwaita kwa uwazi,


ثُمَّ إِنِّيٓ أَعۡلَنتُ لَهُمۡ وَأَسۡرَرۡتُ لَهُمۡ إِسۡرَارٗا

Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.


فَقُلۡتُ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ إِنَّهُۥ كَانَ غَفَّارٗا

Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.


يُرۡسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡكُم مِّدۡرَارٗا

Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.


وَيُمۡدِدۡكُم بِأَمۡوَٰلٖ وَبَنِينَ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ جَنَّـٰتٖ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ أَنۡهَٰرٗا

Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.


مَّا لَكُمۡ لَا تَرۡجُونَ لِلَّهِ وَقَارٗا

Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?


وَقَدۡ خَلَقَكُمۡ أَطۡوَارًا

Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?


أَلَمۡ تَرَوۡاْ كَيۡفَ خَلَقَ ٱللَّهُ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖ طِبَاقٗا

Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?


وَجَعَلَ ٱلۡقَمَرَ فِيهِنَّ نُورٗا وَجَعَلَ ٱلشَّمۡسَ سِرَاجٗا

Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?



الصفحة التالية
Icon