وَبَنِينَ شُهُودٗا

Na wana wanao onekana,


وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا

Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.


ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ

Kisha anatumai nimzidishie!


كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!


سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا

Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.


إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.


فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!


ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!


ثُمَّ نَظَرَ

Kisha akatazama,


ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Kisha akakunja kipaji, na akanuna.


ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ

Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.



الصفحة التالية
Icon