وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Bali alikanusha, na akageuka.


ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.


أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ

Ole wako, ole wako!


ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ

Kisha Ole wako, ole wako!


أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?


أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?


ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.


فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.


أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?



الصفحة التالية
Icon