كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!


هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,


وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!


هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.


فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!


وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!


إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,


وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda wanayo yapenda,



الصفحة التالية
Icon