لِّلطَّـٰغِينَ مَـَٔابٗا

Kwa walio asi ndio makaazi yao,


لَّـٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا

Wakae humo karne baada ya karne,


لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا

Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,


إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا

Ila maji yamoto sana na usaha,


جَزَآءٗ وِفَاقًا

Ndio jaza muwafaka.


إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا

Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.


وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا

Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.


وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.


فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!


إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا

Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,


حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا

Mabustani na mizabibu,



الصفحة التالية
Icon