وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا

Na milima akaisimamisha,


مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.


فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,


يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,


وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,


فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,


وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akakhiari maisha ya dunia,


فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!


وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,


فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!



الصفحة التالية
Icon