وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.


وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.


وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ

Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.


فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ

Basi mnakwenda wapi?


إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.


لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ

Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.


وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.



الصفحة التالية
Icon