كِرَامٗا كَٰتِبِينَ

Waandishi wenye hishima,


يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ

Wanayajua mnayo yatenda.


إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,


وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;


يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Wataingia humo Siku ya Malipo.


وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ

Na hawatoacha kuwamo humo.


وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?


ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?


يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ

Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.



الصفحة التالية
Icon