وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمۡ يَتَغَامَزُونَ

Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.


وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓاْ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمُ ٱنقَلَبُواْ فَكِهِينَ

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.


وَإِذَا رَأَوۡهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.


وَمَآ أُرۡسِلُواْ عَلَيۡهِمۡ حَٰفِظِينَ

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.


فَٱلۡيَوۡمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنَ ٱلۡكُفَّارِ يَضۡحَكُونَ

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,


عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.


هَلۡ ثُوِّبَ ٱلۡكُفَّارُ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?



الصفحة التالية
Icon