وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,


ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Ambaye atauingia Moto mkubwa.


ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ

Tena humo hatakufa wala hawi hai.


قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.


وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.


بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!


وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.


إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,


صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.



الصفحة التالية
Icon