كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,


وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,


وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?


يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!


فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.


وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.


يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!


ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.


فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,



الصفحة التالية
Icon