وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?


فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;


أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ

Au kumlisha siku ya njaa


يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ

Yatima aliye jamaa,


أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ

Au masikini aliye vumbini.


ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.


أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.


وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.


عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.



الصفحة التالية
Icon