إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ

Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.


وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.


فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!


لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى

Hatauingia ila mwovu kabisa!


ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Anaye kadhibisha na kupa mgongo.


وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى

Na mchamngu ataepushwa nao,


ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.


وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.


إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.


وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ

Naye atakuja ridhika!



الصفحة التالية
Icon