قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ

Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?


قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ

Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.


قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ

Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?


قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?


قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!


إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.


إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.


فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,



الصفحة التالية
Icon