قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?


قَالَ هَـٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ

Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.


لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.


فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ

Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.


فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ

Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.


إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ

Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.


وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ

Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.


إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.


وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ

Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.



الصفحة التالية
Icon