ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.


قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,


وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na unifanyie nyepesi kazi yangu,


وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,


يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu.


وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,


هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu.


ٱشۡدُدۡ بِهِۦٓ أَزۡرِي

Kwake yeye niongeze nguvu zangu.


وَأَشۡرِكۡهُ فِيٓ أَمۡرِي

Na umshirikishe katika kazi yangu.


كَيۡ نُسَبِّحَكَ كَثِيرٗا

Ili tukutakase sana.


وَنَذۡكُرَكَ كَثِيرًا

Na tukukumbuke sana.



الصفحة التالية
Icon