قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.


فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.


وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.


قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.


يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?


قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.


يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.


فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.



الصفحة التالية
Icon