فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.


إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.


وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Nao wanatuudhi.


وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.


فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,


وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na makhazina, na vyeo vya hishima,


كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.


فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ

Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.


فَلَمَّا تَرَـٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ

Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!


قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!



الصفحة التالية
Icon