فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.


۞قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ

Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?


قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?


إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ

Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!


وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.


إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.


قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.


قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.


فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.



الصفحة التالية
Icon