أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ

Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?


وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ

Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!


وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ

Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.


فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.


وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ

Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.


أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ

Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.


وَجَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ

Na mabustani na chemchem.


إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.


قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ

Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.



الصفحة التالية
Icon