أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?


فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani, na chemchem?


وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ

Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.


وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.


فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.


وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,


ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ

Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.


قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.


مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.



الصفحة التالية
Icon