ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ

Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,


مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ

Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?


وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ

Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -


ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.


وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ

Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,


وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ

Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.


إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ

Hakika hao wametengwa na kusikia.


فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ

Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.


وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ

Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.



الصفحة التالية
Icon