فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ

Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!


وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.


هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.


۞ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ

Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -


مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ

Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!


وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ

Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:


مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ

Mna nini? Mbona hamsaidiani?


بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ

Bali hii leo, watasalimu amri.


وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.



الصفحة التالية
Icon