إِنَّهَا شَجَرَةٞ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ

Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.


طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ

Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.


فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.


ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبٗا مِّنۡ حَمِيمٖ

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.


ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.


إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ

Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.


فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ

Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.


وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.


وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ

Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.



الصفحة التالية
Icon