مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ

Mna nini hata hamsemi?


فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.


فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ

Basi wakamjia upesi upesi.


قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?


وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!


قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!


فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.


وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.


رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.



الصفحة التالية
Icon