فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;


إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.


وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.


سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ

Iwe salama kwa Ilyas.


إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.


إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.


وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.


إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,


إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.


ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengineo.



الصفحة التالية
Icon