وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.


وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.


وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ

Na walikuwapo walio kuwa wakisema:


لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,


لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.


فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.


وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.


إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.


وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.


فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Basi waachilie mbali kwa muda.



الصفحة التالية
Icon