مُتَّكِـِٔينَ فِيهَا يَدۡعُونَ فِيهَا بِفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ وَشَرَابٖ

Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.


۞وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ أَتۡرَابٌ

Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.


هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوۡمِ ٱلۡحِسَابِ

Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.


إِنَّ هَٰذَا لَرِزۡقُنَا مَا لَهُۥ مِن نَّفَادٍ

Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.


هَٰذَاۚ وَإِنَّ لِلطَّـٰغِينَ لَشَرَّ مَـَٔابٖ

Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;


جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَا فَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.


هَٰذَا فَلۡيَذُوقُوهُ حَمِيمٞ وَغَسَّاقٞ

Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!


وَءَاخَرُ مِن شَكۡلِهِۦٓ أَزۡوَٰجٌ

Na adhabu nyenginezo za namna hii.


هَٰذَا فَوۡجٞ مُّقۡتَحِمٞ مَّعَكُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِهِمۡۚ إِنَّهُمۡ صَالُواْ ٱلنَّارِ

Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.



الصفحة التالية
Icon