إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.


إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Hakika Mti wa Zaqqum,


طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ

Ni chakula cha mwenye dhambi.


كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni


كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ

Kama kutokota kwa maji ya moto.


خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!


ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ

Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.


ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!


إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.


إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,



الصفحة التالية
Icon