يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?


يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ

Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.


ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ

Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.


إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.


ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُحۡسِنِينَ

Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.


كَانُواْ قَلِيلٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مَا يَهۡجَعُونَ

Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.


وَبِٱلۡأَسۡحَارِ هُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ

Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.


وَفِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.


وَفِي ٱلۡأَرۡضِ ءَايَٰتٞ لِّلۡمُوقِنِينَ

Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.



الصفحة التالية
Icon