أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?


وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na akamwona mara nyingine,


عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Penye Mkunazi wa mwisho.


عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.


إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.


مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.


لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.


أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je! Mmemuona Lata na Uzza?


وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaat, mwingine wa tatu?


أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?



الصفحة التالية
Icon