وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ

Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.


فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Vikaifunika vilivyo funika.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?


هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ

Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.


أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ

Kiyama kimekaribia!


لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.


أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ

Je! Mnayastaajabia maneno haya?


وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ

Na mnacheka, wala hamlii?


وَأَنتُمۡ سَٰمِدُونَ

Nanyi mmeghafilika?


فَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ وَٱعۡبُدُواْ۩

Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.



الصفحة التالية
Icon