إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ

Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.


وَمَآ أَمۡرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٞ كَلَمۡحِۭ بِٱلۡبَصَرِ

Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.


وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَآ أَشۡيَاعَكُمۡ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?


وَكُلُّ شَيۡءٖ فَعَلُوهُ فِي ٱلزُّبُرِ

Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.


وَكُلُّ صَغِيرٖ وَكَبِيرٖ مُّسۡتَطَرٌ

Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.


إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَهَرٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.


فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ

Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.



الصفحة التالية
Icon