يَخۡرُجُ مِنۡهُمَا ٱللُّؤۡلُؤُ وَٱلۡمَرۡجَانُ

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


وَلَهُ ٱلۡجَوَارِ ٱلۡمُنشَـَٔاتُ فِي ٱلۡبَحۡرِ كَٱلۡأَعۡلَٰمِ

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


كُلُّ مَنۡ عَلَيۡهَا فَانٖ

Kila kilioko juu yake kitatoweka.


وَيَبۡقَىٰ وَجۡهُ رَبِّكَ ذُو ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


يَسۡـَٔلُهُۥ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ كُلَّ يَوۡمٍ هُوَ فِي شَأۡنٖ

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?



الصفحة التالية
Icon