فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُسۡـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٞ وَلَا جَآنّٞ

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


يُعۡرَفُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ بِسِيمَٰهُمۡ فَيُؤۡخَذُ بِٱلنَّوَٰصِي وَٱلۡأَقۡدَامِ

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.


يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.


فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?


وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.



الصفحة التالية
Icon