Yasin


يسٓ

Ya-Sin (Y. S.).


وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡحَكِيمِ

Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!


إِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,


عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Juu ya Njia Iliyo Nyooka.


تَنزِيلَ ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.


لِتُنذِرَ قَوۡمٗا مَّآ أُنذِرَ ءَابَآؤُهُمۡ فَهُمۡ غَٰفِلُونَ

Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.


لَقَدۡ حَقَّ ٱلۡقَوۡلُ عَلَىٰٓ أَكۡثَرِهِمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.


إِنَّا جَعَلۡنَا فِيٓ أَعۡنَٰقِهِمۡ أَغۡلَٰلٗا فَهِيَ إِلَى ٱلۡأَذۡقَانِ فَهُم مُّقۡمَحُونَ

Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.


وَجَعَلۡنَا مِنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ سَدّٗا وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ سَدّٗا فَأَغۡشَيۡنَٰهُمۡ فَهُمۡ لَا يُبۡصِرُونَ

Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.



الصفحة التالية
Icon