At-Tur


وَٱلطُّورِ

Naapa kwa mlima wa T'ur,


وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na Kitabu kilicho andikwa


فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika ngozi iliyo kunjuliwa,


وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na kwa Nyumba iliyo jengwa,


وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,


وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na kwa bahari iliyo jazwa,


إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.


مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia.


يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,


وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.


فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,



الصفحة التالية
Icon