Al-Waki'ah


إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Litakapo tukia hilo Tukio


لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.


خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Literemshalo linyanyualo,


إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,


وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima itapo sagwasagwa,


فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,


وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-


فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?


وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?


وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na wa mbele watakuwa mbele.


أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao karibishwa



الصفحة التالية
Icon