Al-Hakkah


ٱلۡحَآقَّةُ

Tukio la haki.


مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Nini hilo Tukio la haki?


وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?


كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.


فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.


وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.


سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.


فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?


وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ

Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.



الصفحة التالية
Icon