Al-Muzzammil


يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُزَّمِّلُ

Ewe uliye jifunika!


قُمِ ٱلَّيۡلَ إِلَّا قَلِيلٗا

Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!


نِّصۡفَهُۥٓ أَوِ ٱنقُصۡ مِنۡهُ قَلِيلًا

Nusu yake, au ipunguze kidogo.


أَوۡ زِدۡ عَلَيۡهِ وَرَتِّلِ ٱلۡقُرۡءَانَ تَرۡتِيلًا

Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.


إِنَّا سَنُلۡقِي عَلَيۡكَ قَوۡلٗا ثَقِيلًا

Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.


إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيۡلِ هِيَ أَشَدُّ وَطۡـٔٗا وَأَقۡوَمُ قِيلًا

Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.


إِنَّ لَكَ فِي ٱلنَّهَارِ سَبۡحٗا طَوِيلٗا

Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.


وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلٗا

Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.


رَّبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ فَٱتَّخِذۡهُ وَكِيلٗا

Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.



الصفحة التالية
Icon