Al-Buruj


وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!


وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ

Na kwa siku iliyo ahidiwa!


وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!


قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ

Wameangamizwa watu wa makhandaki


ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,


إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ

Walipo kuwa wamekaa hapo,


وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.


وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,


ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.



الصفحة التالية
Icon