Al-Ghashiyah


هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?


وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,


عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ

Zikifanya kazi, nazo taabani.


تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ

Ziingie katika Moto unao waka -


تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.


لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.


لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.


وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.


لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,


فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani ya juu.


لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ

Hawatasikia humo upuuzi.



الصفحة التالية
Icon