Al-Fajr


وَٱلۡفَجۡرِ

Naapa kwa alfajiri,


وَلَيَالٍ عَشۡرٖ

Na kwa masiku kumi,


وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,


وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ

Na kwa usiku unapo pita,


هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?


أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?


إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu?


ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?


وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?


وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi?


ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi?



الصفحة التالية
Icon