Al'Alak


ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,


خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,


ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!


ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ

Ambaye amefundisha kwa kalamu.


عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.


كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri


أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ

Akijiona katajirika.


إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.


أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ

Umemwona yule anaye mkataza


عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ

Mja anapo sali?


أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?



الصفحة التالية
Icon