At-Tahrim
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَآ أَحَلَّ ٱللَّهُ لَكَۖ تَبۡتَغِي مَرۡضَاتَ أَزۡوَٰجِكَۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Ewe Nabii! Kwa nini unaharimisha alicho kuhalilishia Mwenyezi Mungu? Unatafuta kuwaridhi wake zako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ewe Mtume! Mbona unajizuia nafsi yako na halali Aliyokuhalalishia Mwenyezi Mungu kwa kuwa unataka kuwaridhisha wake zako? Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kukusamehe, ni Mwenye huruma kwako.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس