إِن تَتُوبَآ إِلَى ٱللَّهِ فَقَدۡ صَغَتۡ قُلُوبُكُمَاۖ وَإِن تَظَٰهَرَا عَلَيۡهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ هُوَ مَوۡلَىٰهُ وَجِبۡرِيلُ وَصَٰلِحُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ بَعۡدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ
Kama nyinyi wawili hamkutubia kwa Mwenyezi Mungu, basi nyoyo zenu zimekwisha elekea huko. Na mkisaidiana dhidi yake (Mtume), basi hakika Mwenyezi Mungu ndiye kipenzi chake, na Jibrili, na Waumini wema, na zaidi ya hayo Malaika pia watasaidia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Iwapo mtarudi kwa Mwenyezi Mungu (ewe Hafsah na 'Aishah) basi yatakuwa yamepatikana kwenu yanayopelekea kukubaliwa toba yenu, kwa kuwa nyoyo zenu zilielekea kwenye kuyapenda yale aliyoyachukia Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ya kutoa siri yake. Na mtakaposaidiana juu yake kwa kufanya yanayomuudhi, basi Mwenyezi Mungu Ndiye Msimamizi wake na Mtetezi wake na Jibrili na Waumini wema. Na Malaika, baada ya usaidizi wa Mwenyezi Mungu, ni wasaidizi wake na watetezi juu ya yoyote anayemuudhi na kumfanyia uadui.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس